skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Tanzania na India zimekubaliana kuendeleza ushirikiano katika nyanja mbalimbali hususani sekta ya elimu ili kuinua kiwancho na ubora wa elimu baina ya Tanzania na India yenye utajiri wa teknolojia ukilinganisha na Tanzania.

Picha ya washiriki wa majadiliano juu ya mashirikiano ya Tanzania na India katika ukuaji wa teknolojia

Hayo yamejadiliwa leo na Waziri wa Elimu wa Tanzania Profesa Joyce Ndalichako wakati akifanya mazungumzo na Balozi wa India nchini Tanzania Bw. Shri Binaya Pradhan wakiwa katika maadhimisho ya siku ya kuenzi ushirikiano wa kiteknolojia na kiuchumi kati ya Tanzania na India yaliyofanyika tarehe 15/9/2021 jijini Dar es salaam

Profesa Joyce Ndalichako- Waziri wa elimu na mafunzo ya Ufundi

Waziri wa Elimu Prof Joyce Ndalichako amemshukuru Balozi Paradhan kwa namna nchi yake ya India inavyotoa ushirikiano mkubwa katika sekta ya elimu na teknolojia kwa tanzania ikiwemoo watanzania kuapata fursa ya elimu nchini India.

Balozi wa India nchini Tanzania Mhe. Shri Binaya Pradhan akiwa na Waziri wa elimu Prof. Joyce Ndalichako wakitoka katika ukumbi wa mikutano jijini Dar es salaam
Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma