skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Na Anita Balingilaki, Simiyu

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa leo anatarajiwa kuzindua mkakati rasmi wa kisekta wa mapambano dhidi ya kifua kikuu ambapo wizara mbalimbali zinashirikishwa katika mapambano hayo.

Hayo hayo yamebainishwa na mratibu wa kitaifa wa masuala ya uraghibishi, mawasiliano na uhamasishaji kutoka mpango wa taifa wa kifua kikuu na ukoma katika wizara ya afya Bw. Julius Mtemahanji huku akiongeza kuwa jambo jingine atakalolifanya mhe, Waziri Mkuu ni kukagua mabanda ya utekelezaji wa afua za kifua kikuu nchini.

Mkakati huo unatarajiwa kuzinduliwa kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya kupambanana kifua kikuu duniani ambapo kitaifa utazinduliwa kwenye viwanja vya halmashauri ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.

Baadhi ya maafisa kutoka Wizara ya afya waliofasili mkoani Simiyu kwa ajili ya siku ya kifua kikuu kitaifa

Kuhusu sababu za maadhimisho hayo kufanyika mkoa wa Simiyu Mtemahanji amesema, mkoa huo unafanya vizuri katika harakati za mapambano dhidi ya kifua kikuu na kwa namna hiyo kama taifa linatambua mchango mkubwa wa mkoa huo na hivyo ni vema shughuli hiyo ikafanyika mkoani hapo.( Simiyu)

Mtemahanji amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo inasema ” kwa pamoja tunaweza kutokomeza kifua kikuu nchini Tanzania” kwahiyo ni wajibu wa kila mtanzania kuja pamoja katika kuhakikisha kwamba mapambano ya kifua kikuu yanafanikiwa.

Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma