skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Na. Felister Nestory Matinde -Mwanza

Katika kuelekea kilele Cha siku ya familia duniani ambayo huadhimishwa Mei 15 kila mwaka, jamii imeshauriwa  itambue haki za watoto na wanawake ambao wamekuwa ni daraja la kufanyiwa vitendo vya ukatili.

Wito huo umetolewa na Mkurugenz mtendaji wa taasisi ya  Haki Zetu iliyopo Nyasaka wilaya ya Ilemela jiji Mwanza  Bw. Gervas Evodius wakati wa mahojiano maalumu na Buha FM Jijini Mwanza kuelekea uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya familia

Akijibu hoja kuhusu watoto wengi kuishi katika mazingira hatarishi jijini Mwanza na sababu za wazazi wao kutowachukua, Bw. Evodius ametaja kuwa migogoro mingi isiyotatuliwa kwa wakati katika familia ni chanzo cha ongezeko la watoto wa mtaani na amesisitiza kuwa jamii inatakiwa iachane na ukatili unaofanywa  dhidi ya watoto na wanawake na jamiii pia kutambua haki ya mtoto wa kike.

Bw. Evodius amesema kuwa ukatili huo unaanzia katika ngazi ya familia kwenda kwenye jamiii hali ambayo inatishia maisha ya wanawake na watoto kwa ujumla na kusababisha kutokujiamini na kupunguza upendo ambao ndio msingi wa familia.

“Sisi Kama taasisi  ya Haki Zetu ambayo inajihusishana kutetea Haki za watoto vijana na wanawake Mara nyingi tumekuwa tukikutana na visa lakini wakati mwingine inakuwa ni vigumu  kuchukua  hatua za kisheria sababu Kuna wazazi wengine wanapoteza ushahidi pamoja na  kuelimisha jamii kuhusu vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto na wanawake na jamii kutokufumbia macho vitendo hivyo viovu”amesema Director Evodius.

Imeelezwa kuwa sababu za ukatili ikiwa pamoja na mlengwa kupitia ukatili zinatokana kulipiza kisasi,mabadiliko ya technolojia na mwingiliano wa tamaduni za magharibi hali  ambayo inayochochea vitendo vya ukatili na unyanyasaji.

“Tunao vijana 190 kwenye shule tofauti na kutoka mikoa mbalimbali Kama shinyanga,geita na Mwanza ambao wanaishi kwenye mazingira magumu na  tunawapatia elimu, tunawalipia ada pamoja na kuwalipia bima za afya ambayo lengo ni kusaidia familia na kuwapa mitaji  midogo midogo halli ambayo itasaidia kujikwamua kiuchumi” amesema Mkurugenz Evodius.

Hata hivyo ameihasa jamii kuachana na vitendo vya ukatili ambavyo vimekuwa viikitishia maisha ya watoto na wanawake,jamii inatakiwa ivunje ukimya unaofanywa na baadhi ya watu,kubadilisha baadhi ya sheria ya ndoa  hii itasaidia wanawake na watoto watapata Haki zao na kujua nini Cha kufanya baada yakufanyiwa ukatili pamoja na jamii iachane  Mila potofu za kuozesha watoto wadogo huku wakijua ni kinyume Cha Sheria.

Sambamba na hayo amesema kuwa afya ya uzazi kwa watoto wa kike na akina mama ni muhimu kuwapa elimu ya uzazi hii itasaidia kuondokana na mimba zisizotarajiwa pamoja  na watoto wa kike kubeba mimba chini ya umri wa miaka 18 Hali ambayo ni tishio kwa afya zao.

Wakati huo huo shirika la hilo limeiomba serikali kupunguza gharama za taulo za kike kwa kuweka mkakati wa kusaidia watoto  wasichana wakiwa shuleni ambao wanatoka kaya maskini pamoja na kuwajengea chumba maalum kwa ajili ya kubadilisha taulo za kike shuleni.

Watoto kadhaa waliohojiwa na Buha FM jijini Mwanza kuhusu sababuu za kuishi mitaani katika mazingira hatarishi walitaja kukimbia madhira ya ugomvi baina ya wazazi wao, umaskini pamoja na kukosa upendo miongoni mwa wana familia ikiwemo ushawishi wa kwenda kupata maisha bora mijini.

Kwa upande wake hussen sultan mkazi wa Mecco  mwenye umri wa miaka 26 anasema kuwa kilichompelekea kukimbilia mtaani ni kufukuzwa nyumbani na ndugu baada ya wazazi wake kufariki dunia.

Nae fidelis Amos mkazi wa Mugumu Serengeti mwenye umri wa miaka 13 amesema kuwa kilichompelekea Kuja mtaani ni baada ya baba yake kuachana na mama yake na kuolewa na mume mwingine ambaye amekuwa akimfanyia ukatili na kukumbilia kwa Bibi ambako alikosa mahitaji ya msingi na baadaye aliamua kwenda mjini ambako anaishi bila makazi maalumu.

Baadhi ya watoto wasio na makazi maalumu ambao huishi katika mitaa mbalimbali jijini Mwanza baada ya kuzihama familia zao kutokana na sababu mbalimbali. Picha na Matinde Nestory

Kwa upande wake Bi. Martha Felician mkazi wa Mecco jijini Mwanza amesema wasichana wengii wanaingia katika majukumu ya kifamilia kutokana na kufanyiwa vitendoo vya ukatilii ikiwemo mimba za mapema na ndoa za utotoni ikiwa ni pamoja na kubakwa.

Akitoa ushuhuda Bi. Martha anabainisha kuwa alipata mimba katika umri mdogo suala lililopelekea wazazi kumfukuza nyumbani na kuishi maisha ya shida kutokana na ukatili aliyofanyiwa mpaka kubeba ujauzito ambao umezima ndoto zake.

“Ninawaomba wazazi msiwatenge watoto wenu pindi wanapopata mimba katika umri mdogo badala yake wapatieni msaada wa elimu au msaada wa kifedha ili waweze kujikimu katika maisha  hii itapunguza  kuwa tegemezi, Alisisitiza Martha Felician.

Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma