skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Na. Mwandishi wetu

Tanzania imeahidi kuendelea kuwapokea wahamiaji na waomba hifadhi ambao watakidhi vigezo kutokana na sheria za uhamiaji, sheria za Ukimbizi na sheria za usalama wa nchi

Hayo yamebainishwa kwa nyakati tofauti na Waziri wa mambo ya Ndani ya nchi Mhandisi Hamad Masauni wakati alipotembelea mkoa wa Kigoma na kugagua vituo vinavyotumika kuwapokea, kuwahakiki na kuwasajili waomba hifadhi kutoka jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanaotaja kuikimbia nchi yao kutokana na hali duni ya usalama

Mhe. Masauni alisisitiza kuwa waomba hifadhi wote wanaoingia nchini Tanzania watahojiwa na kuhakikiwa ili kubaini uhalali wa sababu zinazopelekea kuzihama nchi zao na kuingia nchini Tanzania na kuhakikisha wasiostahili kupewa hifadhi wanabainika na kuchukuliwa hatua

Mhandisi Hamad Masauni (aliyefunga mikono kifuani) akisikiliza hoja za waomba hifadhi kutoka DRC waliopokelewa mjini Kigoma. Picha zote na Happiness Tesha

“Tanzania imekuwa na historia nzuri ya kuwapokea raia wa nchi nyingine ambao wanakuja kuomba hifadhi, hivyo tutawapa hifadhi wale watakaostahili na wasio stahili watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria zetu, hatuwezi kuruhusu watu walioingia kinyume cha sheria na kuishi Nyarugusu au katika vijiji watumia fursa ya kuomba hifadhi kuhalalisha makosa yao, tukiwabaini tutawachukulia hatua” alisisitiza Masauni

Waziri Masauni alitembelea pia kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu ambayo inatumika kuhifadhi wakimbizi kutoka Jamhuri ya Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo sambamba na waomba hifadhi wapya kutoka DRC ambao wanaendelea kuhojiwa ili kuwapa uhalali wa kuwa wakimbizi.

Waomba hifadhi kutoka DRC wakisubiri hatima yao wakati zoezi la uhakiki likiendelea kataika ofisi za wizara ya mambo ya ndani idara ya wakimbizi mjini Kigoma. Picha na Happiness Tesha

Zaidi ya waomba hifadhi wapya 6000 wamekwishapokelewa mkkoani Kigoma tangu March 5 mwaka huu wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto.

Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma