Asema ni mpango wa kumtua mama kuni kichwani , Amshukuru Rais Samia Na. Mwandishi wetu…
Na. Mwandishi wetu, Kigoma
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Bi. Mwantum Mgonja Leo Julai 30, 2023 amefanya ziara Soko la Masanga kwa lengo la kukagua miundombinu na ufanisi wa Soko katika kuhudumia Wakazi wa Manispaa hiyo
Katika ziara hiyo Mkurugenzi ameambatana na Mkuu wa divisheni ya Biashara na uwekezaji Bw. Robert Sabhoya na Mwekahazina wa Manispaa Bw. Osward Mwakalasi
Katika ziara hiyo ya kutaathimini uwekezaji na kukagua mazingira ya biashara, Mkurugenzi huyo amekutana na Kuongea na Mwenyekiti wa Soko Ndugu. Jafet John Nayingo ambapo amemuelezea changamoto za soko hilo na kuahidi kuzitatua
Bw. Nayingo amemweleza mkurugenzi kuwa mazingira ya soko ni mazuri japo kuna changamoto ndogo ndogo za uelewa ambazo zinatakiwa kutatuliwa kwa kutoa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu mifumo mbalimbali ya kiserikali
Aidha Mkurugenzi ameongea na mfanyabiashara mmoja mmoja huku akifanya ununuzi wa baadhi ya bidhaa ndani ya soko hilo na kufurahishwa na namna wakazi wa mansapaa ya kigoma wanavyojituma katika kufanya shughuli halali za kjkuza uchumi