skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Na. Matinde Nestory

Wadau wa sekta ya madini wamekutana jijini Mwanza kwenye jukwaa la kwanza la utekelezaji na ushirikishwaji wa watanzania katika sekta ya madini kufuatia mabadiliko ya Sheria ya Madini.

Jukwaa hilo limefanyika Rocky City Mall jijini Mwanza likiongozwa na mwenyekiti wa tume ya madini profesa Idrisa kikula  ambaye amemwakilisha waziri wa Madini  mheshimiwa Doto Biteko

Professa Kikula amesema kuwa sekta ya Madini imefanya  mabadiliko ya Sheria ambayo yamepekekea kutungwa kwa kanuni za ushirikishwaji wa Tanzania za mwaka 2018, na kwamba lengo kuu  ni kuibua na kuchochea kuongezeka kwa fursa mbalimbali za ajira na matumizi ya huduma  na bidhaa zinazozalishwa nchini  Tanzania.

” Katika kipindi Cha kuanzia  mwaka 2018 -2021 sekta ya Madini  imeongeza  kwa kiasi kikubwa kiwango cha ushirikishwaji watanzania katika maeneo mbalimbali ajira na mafunzo kwa watanzania katika migodi mikubwa na Kati ambapo kumekuwepo na ongezeko la ajira  6668  sawa na 95% kwa mwaka 2018  hadi kufikia  14308 sawa na  97%  za mwaka 2021

Profesa Idris Kikula mwenyekiti wa Tume ya Madini nchini Tanzania akitoa maelezo wakati wa kongamano la ushirikishwaji wa wadau wa madini jijini Mwanza

Anasisitiza kuwa ongezeko  hilo la ajira kwa watanzania  limechochewa na usimamizi  wa ushirikishwaji watanzania wamepewa kipaumbele katika fursa za ajira zote  nchini.

Akizungumzia changamoto amesema kuwa baadhi ya makampuni ya kigeni hayajaweza kukidhi matakwa kwa kuingia ubia na wachimbaji wa Tanzania na kwamba hali hiyo imepelekea kampuni za wazawa kokosa sifa, upungufu wa viwanda nchini kwa ajili ya uchimbaji na uchenjuaji nchini, wamiliki wa leseni na watoa huduma kutokutekeleza matakwa ya uchenjuaji kwa kushindwa kufanikisha mpango wa ushirikishwaji, kushindwa kufata taratibu za manunuzi.

Nae Bi. Janeth Reuben ambaye ni kamishna wa ushirikishwaji tume ya madini amesema kuwa tume ya hiyo iko kwa ajili ya kujadili na kujengeana uwezo wa kujua rasilimali dhahabu na Madini mengine na jukwaa hili litakuwa linafanyika kila mwaka ili kujua changamoto zilizopo na kuzipatia ufumbuzi.

Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma