skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Mkuu wa mkoa wa Mwanza  Robert Gabriel amewaomba wananchi kutokomeza ukatili wa kijinsia ambao unaanzia katika ngazi ya familia kwenda kwenye  jamii.

Baadhi ya watoto mkoani Mwanza washiriki maadhimisha ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na wanawake

Ameyasema haya katika maadhimisho ya ukatili wa kijinsia ambayo kitaifa yamefanyika mkoani  Mwanza yenye kauli mbiu “Ewe mwananchi komesha ukatili wa kijinsia sasa”

Madhimisho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Nyamagana jijini humo, yamehudhuriwa na shirika la kutetea haki za wanawake na wasichana la KIVULINI, Plan International,Wote sawa, Railway Children na Source Children Village wote wakiwa na lengo la kutokomeza ukatili wa kijinsia.

RC Gabriel  ametaja mikoa ya Kanda ya ziwa inayoongoza kwa ukatili wa kijinsia ikiongoza mikoa ya Shinyanga na Mara 78%, Kagera 67, Geita 63%, Simiyu 62% na Mwanza asilimia 60%

Kwa upande wake Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani humo  SACP Ramadhani Ng’anzi amesema kuwa siku kumi na sita za kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia jeshi la polisi linapinga ukatili wa  aina yoyote ambao unafanyika dhidi ya wanawake na watoto ambao umeathiri utendaji kazi wao na kutokujiamini  katika kutetea haki zao.

Naye Afisa Mwandamizi wa shirika la kutetea haki za wanawake na wasichana KIVULINI Grace Mussa amesema vitendo vya unyanyasaji wa watoto unatakiwa ushughugulikiwe kwa usiri  kwa masaa ishirini na nne na kwa weledi ili kulinda utu wa watoto.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na ofisi ya taifa ya takwimu NBS mwaka 2015 na 2016 inaonesha  kuwa mikoa  ya kanda ya ziwa inaongoza nchini kwa kiwango kikubwa cha ukatili wa kijinsia.

Mwandishi: Matinde Nestory

Mhariri: Adela Madyane

Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma