skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Na. Mwandishi wetu, KIA

Serikali ya Tanzania imefanikiwa kutatua changamoto ya hitilafuu ya taa za kuongozea ndege katika uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro ambayo ilisababisha wageni walikuwa wakisafiri kwa shirika la ndege la Uholanzi KLM kushushwa katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda

Kwa mujibu wa msemaji mkuu wa serikali Bw. Gerson Msigwa, tukio hilo lilitokea jana majira ya jioni baada ya taa hizo kushindwa kufanya kazi katika kiwango kinachotakiwa na kupelekea usumbufu kwa ndege zilizotakiwa kutua katika uwanja huo

Kuhusu Uvumi wa kufungwa kwa uwanja huo Bw. Msigwa amebainisha kuwa tayari marekebeishoo yamefanyika na ndege zinaendelea kuutumia uwanja huoo kama kawaida na kwamba abiria walioshushwa nchini jirani ya Uganda taratibu za kuwasafirisha kwenda Kilimanjaro zinaendelea

Video hapa chini inafafanua kuhusu taarifa hizo

Msemaji wa Serikali Bw. Gerson Msigwa akitoa ufafanuzi kuhusuu taharuki iliyozuka baada ya changamoto za taa katika uwanja wa KIA
Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma