skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Na ZAKIA  NDULUTE – Kibondo

Chama cha Mapinduzi kimewataka wazazi nchini kuhakikisha Watoto wao wanapata malezi mazuri sambamba na kuhudhuria masomo shuleni ili kudhibiti mmomonyoko wa maadili na kuondokana na wimbi kubwa la watototo mitaani

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya kibondo Comrade Hamisi Tahilo wakati wa ufunguzi wa wiki ya jumuiya ya wazazi iliyofanyika katika kata ya Mabamba  wilayani Kibondo

Tahilo ameongeza kuwa  suala la malezi hafifu limechangia utoro sugu wa watoto na wengi kutoripoti shuleni kwa wakati hali inayohatarisha ustawi wa jamii nchini

Ametoa wito kwa jumuiya ya wazazi kuitumia wiki ya wazazi kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuzingatia malezi bora ya familia hususani Watoto na kuhakikisha taifa linakuwa na raia wema

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kibondo Bw. Hamis Tahilo (wa tatu kushoto) na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kigoma Komredi Jamali Tamim (wa nne kushoto) wakitoa zawadi kwa wanachama wa Jumuiya ya wazazi wilaya ya Kibondo wakati wa wiki ya wazazi katika mji mdogo wa Mabamba

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha mapinduzi  ccm mkoa wa Kigoma  Mh. Jamali Abdallah Tamimu ambaye alihudhuria sherehe hizo kama mkazi wa Mabamba alitumia nafasi ya kusalimu wananchama kwa kuweka bayana kuwa chama cha mapinduzi kimekuwa cha mfano  Afrika kutokana na umahili na umalidadi wake wa kujali maadili na kuwataka  wadau wa chama hicho kuendelea kuwa na ushirikiano mzuri kwa viongozi wao katika kuongeza juhudi za  kuleta maendeleo  bora ya wananchi

Naye mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi wilaya ya kibondo Ndugu Phales Nzobhona  alisema kuwa jumuiya ya wazazi imepata  mafanikio  makubwa ambapo idadi  imeongezeka  kutoka wanachama  6580 hadi kufikia idadi ya wanachama 6602 ambapo wanawake ni 2960 na wanaume ni 3620  pamoja  na wanachama wapya 22 ambao wote ni mchanganyiko

Aidha kwa upande wake katibu wa jumuiya ya wazazi wilaya ya kibondo Ndugu Evarist Msafiri amekemea vitendo viovu vya ukatili kwa watoto na kuwahimiza wazazi kuwa na ushirikano mzuri kwa kuvikemea na kuviripoti pindi vinapotokea katika maeneo yao                                                       

Kila mwaka mwezi APRILI  hufanyika maadhimisho ya wiki ya jumuiya ya wazazi  na kauli mbiu ya mwaka huu ni TAIFA BORA  NI KUTOKANA NA MALEZI BORA YA WATOTO ‘

Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma