skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Na. Matinde Nestory, Mwanza

Waumini wa dini ya kiislam mkoani Mwanza wakiongozwa na Meya wa Jiji la Mwanza wameshiriki siku ya Eid Elftri kwa kutoa  chakula kwa watoto yatima na watoto waishio mazingira magumu

Akifungua sherehe hiyo leo Mstahiki Meya  Constantine Sima amesema kuwa dhamira ni kushiriki chakula Cha pamoja na watoto hao ili inasaidia kuonyesha upendo na mshikamano kwa watoto bila kujali dini zao

Sisi Kama serikali tunatambua na tunawajibu wa kuhakikisha kwamba kundi hilo maalum tuendelea kulitunza na tunaamini kwamba yatima wa leo ni mzazi wa kesho“amesema Meya Sima.

Kwa upande wake Sheikhe Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Hassan Kabeke amesema kuwa hakuna mtaa unaozaa mtoto hivyo tuwatunze watoto tuwapende na kuwathamini watoto hii itasaidia kupunguza ongezeko la watoto wa mtaani. 

“Jamii inatakiwa ikae na watoto yatima majumbani kwetu ni Jambo Bora zaidi lenye baraka zaidi kwa Mungu kuliko kuwalea kwenye vituo na kuwaacha wakizurura mtaani “amesema Sheikhe Kabeke.

Hata hivyo amewataka  waislam kuendelea kuyaishi Yale yote waliyojifunza katika kipindi Cha  mfungo mtukufu wa ramadhani kwa kutoa sadaka kwa wahitaji.

Nae  Mkurugenzi wa Rock solution limited  Zakaria Elias Nzuki amesema kuwa amekuwa akijitolea  kuwasaidia watoto yatima na waishio mazingira magumu kwa Mkoa wa Mwanza na sehemu mbalimbali hii inasaidia kuongeza upendo dhidi ya watoto na anatoa wito kwa viongozi na wadau wengine kuwajali watoto na watu wanaoishi katika mzaingira magumu

“Katika siku Kama hii maalumu huwa tunajitolea kushiriki nao chakula cha pamoja  na kufanya mambo mbalimbali ambayo tumekuwa  tukifanya ni mwaka wa nne mpaka Sasa kila Mwaka mpya na siku ya Eid” amesema  Nzuki.

Aidha amewaomba watu mbalimbali wajitokeze kuwasaidia watoto yatima na waishio mazingira Elimu na Mavazi  hii itasaidia kupunguza wimbi la watoto waishio mtaani.

Mmoja wa watoto waishio mazingira magumu  Joseph Isack Jeremiah kutokea Geita amesema kuwa  changamoto ni nguo ambazo zimekuwa zikiwaishia,Mvua ikinyesha ,kukimbizwa na pa kulala, kufanyiwa ukatili  hali ambayo inatishia afya zao.

Ameiomba jamii kuwasaidia mahitaji mbalimbali ikiwemo kuwapatia  Elimu,Mavazi na Maradhi hii itasaidia kuondoa ongezeko la watoto waishio mtaani.

Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma