skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Huduma ya Radio barani Afrika zimepongezwa kwa namna zinavyotoa huduma za utangazaji na kuzisaidia serikali kuwafikia wananchi sambamba na kudumisha Amani

Hayo yamebainishwa na Naibu waziri wa Habari, mawasiliano nanteknolojia ya habari nchini Tanzania Bw. Kundo Mathew wakati akifungua kongamano la utangazaji la mwaka 2023 jijini Dodoma

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Dodoma Bi. Rosemary Senyamule amekiri kuwa urahisi wa serikali kuifikia jamii ktk masuala mbalimbali ya kijamii, kiuchumu, kiusalama na kisiasa kumekuwa rahisi kutokana na namna waandishi wa habari wa Radio wanavyowasilisha maudhui sambamba na kuaminiwa kwao na urahisi wa jamii kusikiliza radio ukilinganisha na vyombo vingine

Wamiliki na viongozi wa radio nchini Twnzania wao wana maoni gani kuhusu huduma za radio na mchango wake kwa maendeleo? Dr. Godfrey Akigawesa ni mkurugenzi wa Karagwe FM kutoka mkoani Kagera mpakani mwa Uganda na Rwanda ambako Radio ikiwahi kutumika vibaya na kusababisha machafuko nchini Rwanda, yeye anakiri kuwa radio zina mchango mkubwa katika kukuza ustawi wa jamii na usuuhishi

Je! Ni kwa namna gani Radio inachangia kudumisha na kushawishi uwepo wa amani katika mataifa yenye migogoro? Je ! Ipo fursa kwa mataifa yenye migogoro kutumia Radio na kurejesha Amani. Brother Edwin Mpokasye ni kiongozi wa Radio Fadhila inayomilikiwa na shirika la Franciscan la kanisa Katoliki nchini Tanzania

Mwandishi wetu Prosper Kwigize ametuandalia ripoti kuhusu siku ya radio duniani kutoka Dodoma Tanzania. Bofya kwenye picha ili kusikiliza

SIkiliza ripoti ya siku ya radio duniani na mchango wake katika kuduiasha amani barani Afrika kama ilivyoandaliwa na Prosper Kwigize kutoka Dodoma

Siku ya Radio duniani huadhimishwa kila mwaka Feb 13 kama sehemu ya azimio la umoja wa mataifa na siku hii inaratibiwa na shirika la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO

Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma