skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Na. Mwandishi wetu,, Ikulu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko ya vituo kwa Mabalozi wawili (02) na uteuzi wa Balozi mmoja (01) kama ifuatavyo: 

  1. Amempangia Balozi Humphrey Herson Polepole kuiwakilisha Tanzania nchini Cuba.  Kabla ya uteuzi huu Balozi Polepole alikuwa Balozi wa Tanzania, nchini Malawi.
Balozi Humphrey Polepole akiwa na Rais Dr. Samia Suluhu Hassan alipoteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi
  •  Amemteua Balozi Lt. Jenerali (mstaafu) Yacoub Mohamed kuiwakilisha Tanzania katika Falme za Kiarabu (UAE).  Kabla ya uteuzi huu, Balozi Mohamed alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Uturuki.

Uteuzi na kupangiwa Kituo

  • Amemteua Bw. Iddi Seif Bakari kuwa Balozi na kumpangia Ubalozi nchini Uturuki. Kabla ya uteuzi huu, Bw. Bakari alikuwa Konseli Mkuu, Dubai.

Tarehe ya uapisho wa Balozi Bakari itatangazwa baadae. 

Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma