skip to Main Content
Simu: +255 653 200 211 | Barua Pepe: info@buhafmradio.co.tz  

Mwenyekiti wa jumuiya ya CCM ya Umoja wa wazazi mkoa wa Kigoma Dr. Nicholaus Zacharia amezuru na kukagua mradi wa kitegauchumi cha chama cha mapinduzi wilaya ya Kibondo baada ya kuombwa na mwenyekiti wa CCM wilayani humo

Ziara hiyo ya kushitukiza imefanyika jana wakatii mwenyekiti wa wazazi akitokea mkoani Kagera kuhani msiba wa mama wa Katibu wa Wazazi wilaya ya Buhigwe aliyefariki wiki iliyopita

Akizuru mradi wa maduka na kituo cha burudani kinachojengwa mkabara la makao makuu ya CCM wilaya ya Kibondo, Dr. Zacharia amepongeza uongozi wa chama wilayani humo kwa kuwa wabunifu na kutoa ushauri kwa wilaya nyingine kamatii za siasa zibuni miradi ya kukitegemeza chama.

Mwenyekiti wa wazazii Mkoa wa Kigoma Dr. Nicholaus Zacharia (katikati) akiwa na viongozi wa CCM wilaya ya Kibondo. kutoka Kulia ni Comrade Sumaye katibu wa CCM (w), Ndugu Hamis Tahiro mwenyekiti wa CCM (w) Ndg Grace Mbwiliza katibu wa UWT na Ndugu Evarist Msafiri katibu wa WAZAZI

Dr. Zacharia amesema, chama kinatakiwa kuwa na miradii ya maendeleo ambayo itatumika katika kuongeza mapato na kukiwezesha pia kumudu gharama za uendeshaji wa majukumu ya chama na kuwatumikia wanachama na kuisimamia serikali

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kibondo Bw. Hamis Tahiro amemweleza mwenyekitii wa Wazazi kuwa kamatii ya siasa ya halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Kibondo imejiwekeza utaratibu wa kubuni miradii mipya na kuendeleza miradi ya zamani ili kukipa mapatoo chama na kuiwezesha ofisi ya wilaya hiyo kujitegemea

Sehemu ya Mradii wa ujenzi wa maduka katika eneoo la CCM wilaya ya Kibondo

Naye katibu wa CCM wilaya ya Kibondo Bw. Raphael Sumaye pamoja nakumshukuru Dr. Zacharia kukubali kutembelea mradi wa CCM wilaya ya Kibondo nje ya ratiba, amemtaja kama kiongozi mahili na mshauri mzuri katika masuala ya ujenzii wa chama na kujitegemea

Sumaye amemuomba mwenyekiti wa wazazi kuwa balozi wao kwa wadau wa maendeleo ili waendelee kukiunga mkono chama cha mapinduzi katika jitihada zake za kuwaletea maendeleo wanachama wake na watanzania kwa ujumla.

Back To Top
Buha FM · Buha FM Radio Sauti Ya Kigoma